6th December, 2019
Tukisalia kwenye taarifa za mafuriko, wakazi wa kijiji cha Gathiriga eneo bunge la kipipiri katika kaunti ya Nyandarua wamepoteza makazi yao baada ya mto Turasha kuvunja kingo zake kufuatia mvua kubwa inayozidi kunyesha. Mafuriko hayo yameacha familia zaidi ya nane bila makao na kuleta uharibifu mkubwa wa mimea pamoja na chakula.