.
25th November, 2019
Uchunguzi unaendelea kubaini kiini cha Kifo cha wakili Sammy Anyanzwa aliyeanguka hadi kufa kutoka jengo la Uhuru na Kazi mjini Mombasa.
Kufikia sasa haijabainika iwapo wakili huyo alirushwa kutoka orofa hiyo ama alijiangusha. Aidha familia inasisitiza kuwa Anyanzwa hakuripoti kuhusu tishio lolote kwa maisha yake na alikuwa akiishi kwa furaha. Je wakili huyo aliuawa ama alijirusha?