25th November, 2019
Serikali Ya Kaunti Ya Lamu Imewekwa Kwenye Kikaango Na Kulaumiwa Vikali Kwa Kushindwa Kuandaa Tamasha Za Kila Mwaka Za Utamaduni Wa Lamu. Tamasha Za Mwaka Huu Za Awamu Ya Kumi Na Tisa Zilifaa Kufanyika Mwezi Huu Wa Kumi Na Moja Ila Hazikuwa. Aliyekuwa Gavana Wa Lamu Issa Timammy Alisema Kuwa Ni Aibu Kubwa Kwa Wakaazi Wa Lamu Kwa Kushindwa Kuandaa Tamasha Hizo Ambazo Huwaleta Watalii Wa Ndani Na Hata Wa Kigeni Kujionea Maeneo Hayo Ya Kitalii Yanayotambuliwa Na Shirika La Umoja Wa Mataifa La Elimu Utamaduni Na Turadhi La Unesco.Aidha Timammy Alimkashifu Gavana Fahim Twaha Kwa Kushindwa Namaadilizi Hayo Na Kumuomba Ampe Nafasi Ya Kuandaa Tamasha Hizo Mwakani Kwa Ajili Ya Maandalizi Ya Kuadhimisha Miaka 20 Tangu Kuasisiwa Kwa Tamasha Hizo.