.
27th January, 2019
Shughuli ya kumtafuta mama mmoja wa umri wa miaka 45 katika kijiji cha wereri eneo bunge la Mbeere ya kaskazini huko Meru, iliingia siku ya tatu kufuatia hofu kuwa huenda alishambuliwa na mamba kando mwa mto Tana.
Inadaiwa mwanamke huyo alikua akiteka maji mtoni kabla ya kuvamiwa pamoja na punda wake.
Kama anavyoarifu Ali Manzu, wanakijiji wanaishi kwa hofu baada ya matukio mingine kama hayo kuripotiwa awali.