14th January, 2019
Mvulana aliyeandikisha matokeo bora zaidi katika mtihani wa kitaifa kwa wanafunzi wa darasa la nane katika shule ya msingi ya AIC Sirgoi kaunti ya Uasin Ngishu mwaka uliopita amelazimika kurejea katika maisha ya kurandaranda mitaani baada ya mtu aliyejitolea kumfadhili kuendelea na masomo ya shule ya upili kujiondoa. Sasa Eliud Kipkosgei amelazimika kurejelea maisha ya awali ya kuchuana na wavulana wanaorandaranda katika mitaa ya mji wa Eldoret baada ya kushindwa kujiunga na shule ya upili licha ya kupata nafasi katika shule ya upili ya Tambach