2nd January, 2019
Aliyekua mchezaji wa timu ya taifa Harambee Stars Dennis Oliech amesajiliwa na mabingwa watetezi wa ligi kuu ya kandanda humu nchini Gor Mahia. Mara ya mwisho kwa Oliech kuicheza kandanda kwa klabu ya hadhi ya juu ilikua ni mwaka 2015 alipojiunga na timu ya Dubai CSC. Kutokana na usajili huo Oliech atakua mojawapo ya wachezaji wanaolipwa zaidi nchini kwenye ligi kuu ya kandanda. Taarifa kutoka kwa klabu ya Gor Mahia zinasema kwamba atazinduliwa hivi karibuni.