18th December, 2018
Bodi ya kutathmini ubora wa filamu nchini KFCB imetoa wito kwa wazazi kuwamakini na watoto wao kila wanapowaomba ruhusa ya kwenda kutazama filamu. Mkuu wa KFCB Tawi la Pwani Bonventure Kioko alisema kuwa watoto wengi wanaruhusiwa kutazama filamu za watu wazima kinyume cha kanuni na masharti ya bodi hiyo. Aidha Bonventure anasema kuwa katika eneo la Malindi wameidhinisha mabaanda 56 ya video lakini mengi hukiuka sheria na muongozo waliopewa na kuanza kuwaharibu maadhili watoto wadogo. Tayari vituo vitatu vya video katika eneo la Malindi, Gongoni na Kisumu ndogo vimepokonywa leseni.