.
16th December, 2018
Wito umetolewa kwa idara ya mahakama na asasi nyingine za serikali kuweka mikakati na taratibu za kuwezesha kuwaachilia huru wafungwa waliokaa gerezani kwa muda mrefu na kuonesha dalili za kurekebika.
Wito huo umetolewa na aliyekuwa mwakilishi wa kike katika kaunti ya Nakuru, Mary Mbugua, alipowaongoza wanawake wa kanisa la pcea kuwatembelea wafungwa katika gereza la wanawake la Lang’ata na kuwapa zawadi za krismasi.
Aidha mbunge huyo wa zamani aliongeza kwamba ni lazima jamii iwe hiari kuwakubali tena wafungwa pindi wanapokamilisha vifungo vyao na kurejea nyumbani.