16th December, 2018
Waziri wa utalii na wanyama pori Najib Balala ameliamuru shirikka la wanyama pori KWS kuwaajiri watu wa familia za walinzi wa wanyama pori waliopoteza maisha yao katika vita dhidi ya uwindaji haramu au kuuawawa na wanyama hao.
Akizungumza hivi leo katika hafla ya kuwaenzi mashujaa wa ulinzi wa mbuga za wanyama pori nchini, mke wa rais Bi Margaret Kenyatta amewapa kongole walinzi wote wanaojitolea kuhakikisha wanyama pori na binadam wanatangamana ipasavyo na pia kuendeleza vita dhidi ya ujangili.