.
27th November, 2018
Mbunge wa igembe kusini Paul Mwirigi leo asubuhi alifikishwa mahakamani huko Meru akikabiliwa na makosa ya kuwazuia polisi kufanya kazi yao na pia kumsaidia mfungwa kutoroka. Mahakama iliarifiwa kwamba hapo jana mbunge huyo aliwazuia polisi kutekeleza majukumu yao kwenye msako wa magari yanayokiuka kanuni za barabara katika barabara ya Meru?Mikindiri. Aidha alimsaidia kutoroka mahabusu aliyekuwa amekamatwa na maafisa hao. Amekanusha makosa hayo na kuachiliwa kwa dhamana ya shilingi nusu milioni.