13th October, 2018
Wafanyakazi wa kike katika shirika la Standard Group wanayo kila sababu ya kutabasamu baada ya kuzinduliwa rasmi kwa vuguvugu linalonuiya kuangazia maslahi ya kina dada hao na haswa wanapokuwa kazini almaarufu kama ' Standard Group Women Network. Wafanyakzi hao kutoka mabewa mbali mbali nchini ya kampuni ya standard walikongamana katika makao makuu ya afisi hizo huku waliokuwa mia moja wa kwanza kuwasili wakipata mapambo ya bure kabla ya kuanza rasmi kwa warsha hiyo hapo jana. Wanawake hao walitambuliwa kupitia nyimbo, mazungumzo ya kuwapa motisha kutoka kwa baadhi ya akina dada waliokomaa kwenye maeneo yao ya kazi. Afisa mkuu mtendaji wa standard orlando lyomu aliwarai akina dada wa kike kutoona haya katika kuafikia ndoto zao huku changamoto ikitolewa kwa wale waliobobea kwenye nyanja zao kuwa mstari wa mbele kukuza vipawa vinayokuwa. Vuguvugu hili linatarajiwa kuwawezesha akina dada kupitia mafunzo maalum ya kina dada ambayo hufanyika nchini.