.
9th October, 2018
Waziri wa elimu Dr. Amina Mohammed amesisitiza kwamba maandalizi yamekamilika na wako tayari kuanza mitihani ya kitaifa majuma matatu yajayo.
Akizungumza alipofika mbele ya kamati ya bunge kuhusu elimu waziri huyo aidha amesema kwamba takriban wanafunzi 1,800 walio kwenya maeneo yaliyoathirika na machafuko ya kimbari sawa na ubomoaji wa majengo kama vile katika mtaa wa kibra watahamishwa kwenye maeneo jirani ili waweze kufanya mitihani yao. Baadhi ya kaunti zilizoathirika ni pamoja na narok, nakuru na Nairobi.