.
24th September, 2018
Wahudumu wa afya katika kaunti ya Nakuru ambao wamekuwa wakifanya mgomo leo wamefanya maandamano hadi afisi za seneta wa kaunti hiyo susan kihika wakimtaka aingilie kati kile wanachosema ni kushindwa kwa gavana lee kinyanjui kuwalipa marupurupu yao pamoja na kutimiza ahadi za kimkataba kwa zaidi ya miezi mitatu sasa. Wahudumu hao ambao wanajumuisha maafisa wa afya, wauguzi na wataalam wa madawa wamemtaka seneta pamoja na waakilishi katika bunge la kaunti kuwasaidia kuishinikiza serikali ya kaunti kuwalipa madai yao.