×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Mauaji ya mwanamke katika eneo la Kilimani-Nairobi yachunguzwa

21st September, 2018

Maafisa wa usalama wameanzisha uchunguzi kufuatia mauaji ya mwanamke mmoja eneo la Kilimani hapa jijini Nairobi. 

Mwili wa mwanamke huyo anayetambulika kama Monika Kimani ulipatikana na nduguye alhamisi nyumbani kwa mwenda zake.

Nduguye marehemu amesema kuwa alikwenda kumjulia hali Monika na akaupata mwili wake kwenye bafu ukiwa na majeraha ya kisu shingoni. 

OCPD wa Kilimani Michael Mushiri amesema kuwa marehemu aliuwawa kwa njia ya kutatanisha na polisi wameanzisha uchunguzi. 

Mwili wa mwenda zake ulipelekwa katika hifadhi ya maiti ya Chiromo.

.
RELATED VIDEOS