21st September, 2018
Muungano wa kutetea maslahi ya wauguzi nchini umepiga jeki wazo la kugeuza hospitali ya pumwani kuwa ya kitaifa iwapo hiyo ndio njia pekee ya kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo. wakiongozwa na katibu mkuu seth panyako wauguzi hao wamekosoa malumbano kuhusiana na hatua iliyoafikiwa na gavana Mike Sonko jumatatu wakisema kwamba sasa itasaidia kufichua uozo ulio pumwani na hata
kuboresha hali hiyo.