5th September, 2018
Mali ya kampuni ya Sukari ya mumias imeanza kupigwa mnada baada ya kampuni hiyo kushindwa kulipa malimbikizi ya mishahara na madeni ya wafanyikazi wake. Wakulima wa kiwanda hicho wameapa kuzuia mali ya kampuni hiyo kupigwa mnada ikiwemo magari ambayo tayari yameorodheshwa. Kuanzia juzi wakulima wamekuwa wakiwazuia mawakala hao kuingia kiwandani humo kwa madai kuwa wamekiuka makubaliano ya kusubiri malipo hadi kiwanda hicho kipate muthamini.