.
22nd July, 2018
Baadhi ya wabunge wa upinzani sasa wanamtaka rais Uhuru Kenyatta kuzidisha juhudi za vita dhidi ya ufisadi kwa kuhakikisha kwamba kila mtu anayehusishwa na madai ya ulaji rushwa na wizi wa mali ya umma anakabiliwa vilivyo pasi na hofu wala mapendeleo yoyote. Wakizungumza kwenye ibada ya Jumapili katika kanisa moja mtaani Mathare, wabunge hao wakiongozwa na mbunge wa Mathare Anthony Oluoch, walimtaja naibu rais Wiilliam Ruto na washirika wake wa karibu kuwa ni kikwazo kikuu kwenye vita dhidi ya ufisadi