17th July, 2018
Wakazi wa kijiji cha Nzawa Mwingi ya magharibi kaunti ya Kitui hapo jana walimfukuza mhubiri anayedaiwa kumnajisi na kumtia mimba msichana wa miaka kumi na mitano.
Inadaiwa wakazi hao waliojawa na ghadhabu waliamua kuchukua hatua hiyo baada ya mhubiri huyo kutishia kwamba watakufa mmoja baada ya mwengine kwa kumlimbikizia makosa hayo. Aidha inadaiwa kando na msichana huyo, mhubiri huyo amekuwa akiwanajisi watoto wengine katika eneo hilo.