.
9th July, 2018
Mchakato wa kurejesha nchini pesa za wizi zilizohifadhiwa katika nchi za kigeni umeanza huku mataifa ya kenya na uswizi yakitia saini mkataba kwenye harakati za kukabiliana na ufisadi. Kwenye hotuba ya pamoja hii leo katika ikulu ya Nairobi, Rais Uhuru Kenyatta na Rais wa Uswizi Alain Berset walisema mipangilio ya kurejesha fedha hizo ipo tayari.