28th June, 2018
Viongozi wa ligi kuu ya soka nchini Gor Mahia watachuana na Posta Rangers katika raundi ya 16 bora ya michuano ya ngao ya sportpesa. Katika droo ya awamu hiyo ambayo imefanyika hii leo, ulinzi stars watapambana na vihiga united huku mabingwa watetezi AFC Leopards wakipangwa na Mwatate United wanaoshiriki ligi ya daraja la pili nchini. Washindi wa mwaka 2014 Sofapaka watamenyana na Western Stima ugani Kinoru nao Tusker FC wawaalike Bungoma Superstars. Mechi za kwanza zitachezwa tarehe 21 mwezi julai.