19th June, 2018
Polisi huko Donholm wanachunguza kifo cha mmoja wao aliyepatikan nyumbani kwake akiwa amejinyonga Koblo Patrick Macharia kutoka kituo cha polisi cha Soweto alistahili kurejea kazini mnamo jumanne asubuhi baada ya mapumziko. Hata hivyo saa za kuwasili kazini zilipofika wenzake wakakosa kumwona, walikata kauli ya kumpigia simu ili wafahamu hali yake. Lakini baada ya simu zao kukosa kupokelewa, waliamua kwenda nyumbani kwake. Hata hivyo iliwabidi wamsubiri bintiye aje aufungue mlango kwani ulikuwa umefungwa kwa ndani. Baadaye walipigwa na butwaa walipoupata mwili wa mwendazake ukining’inia katika chumba chake cha kulala. Majirani wamemtaja kuwa mtu mpole na mpenda amani. Alikuwa akiishi katika nyumba za polisi za Donholm