.
24th May, 2018
Waziri wa Kilimo Mwangi Kiunjuri ametakiwa kujiuzulu kufuatia sakata ya mahindi katika bodi ya kitaifa ya nafaka na uzalishaji NCPB. Wabunge wa Jubilee Alfred Keter na mwenzake Silas Tiren wamemtaka rais Uhuru Kenyatta kuwajibika na kuhakikisha wote waliohusika kwenye sakata hiyo na ile ya shilingi bilioni 9 katika idara ya huduma ya vijana NYS wamechukuliwa hatua.