.
22nd May, 2018
Maafisa kutoka tume ya maadili na kupambana na ufisadi, EACC, mapema leo waliyavamia makao ya aliyekuwa waziri wa uchukuzi, Michael Kamau, wakiwa na lengo la kumkamata. Hata hivyo maafisa hao waliofika nyumbani kwake Kamau mwendo wa saa kumi na moja alfajiri, waliondoka baada ya kupiga kambi kwa takribani saa tano, baada ya familia na mawakili wake Kamau kukataa kuwakubalia kwa misingi kwamba hawakuwa na stakabadhi za mahakama.