.
1st May, 2018
Kenya imejumuika na mataifa mengine duniani katika kuadhimisha sherehe za leba dei zilizofanyika katika bustani ya Uhuru hapa jijini Nairobi. Katika sherehe hizo serikali imetangaza nyongeza ya mshahara wa chini kwa wafanyikazi wa humu nchini kwa asilimia 5. Kwenye hotuba yake kupitia kwa waziri wa leba Ukuru Yattan Rais Uhuru Kenyatta aliongeza kuwa ni masikitiko makubwa kwamba Kenya ilipoteza saa milioni 100 za utenda kazi katika kipindi cha mwaka uliopita kupitia migomo ya wafanyikazi.