27th April, 2018
Kwenye kila dakika kila mmoja huwa kwenye hatari ya kuwa mgonjwa na hivyo kuhitaji huduma za afya ziwe za dharura au za kawaida. Hivyo basi ipo haja ya bima itakayogharamia matibabu hayo.
Katika mataifa mengine kama vile Canada na Uingereza, bima ya afya hutolewa na serikali kama haki kama ilivyo huduma za polisi au hata elimu ya umma. Kenya ingali haijafika hapo, japo juhudi zinawekwa kufanikisha lengo hilo.