23rd March, 2018
Chama cha walimu nchini KNUT sasa kimetishia kuanzisha mchakato wa kumuondoa afisini afisa mkuu mtendaji wa TSC Nancy Macharia kwa kutochukulia kwa uzito masuala yanayowakumba walimu nchini. Wakiongozwa na katibu mku wa muungano huo Wilson Sossion, knut wamelalamikia hatua ya TSC kufeli kuhudhuria kikao cha leo kati ya TSC na KNUT kilichonuiya kujadili baadhi ya changamoto wanazopitia walimu kisa cha hivi karibuni kikiwa kile kinachozingira walimu kutoka maeneo ya kaskazini mashariki wanaotaka uhamisho.