19th March, 2018
Wakati huo huo tume ya taifa ya kushughulikia haki za binadamu, KNHCR, imemtaka Rais Uhuru Kenyatta kutoidhinisha pendekezo la kupunguza mishahara ya maafisa wa polisi. Mwenyekiti wa tume hiyo, Kagwiria Mbogori, amesema hatua hiyo inakiuka haki za maafisa hao na ni kinyume cha sheria za uajiri. Akizungumza alipokuwa akitoa ripoti ya hali ya haki za binadamu nchini, ameonya kwamba iwapo serikali itaipunguza mishahara ya maafisa wa polisi, huenda idara ya usalama ikatumbukia msukosuko.