13th February, 2018
Chama cha wanahabari wa michezo kimepigwa jeki baada ya kampuni ya LG kutoa ufadhili wa shillingi milioni sita ambazo zitawezesha chama hicho kutuza wachezaji bora kila mwezi katika ligi kuu ya kandanda nchini. Chama hicho kitamtuza mchezaji bora kila mwezi na mchezaji huyo atapokea televisheni. Kampuni hiyo ya LG pia itasaidia chama hicho kuandaa tuzo za mchezaji bora mwishoni mwa msimu.