25th October, 2016
Timu ya Kenya ya voliboli ya chipukizi ilipata ushindi kwenye mechi yake ya tatu baada ya kulaza Senegal seti 3-0 kwenye mechi iliyochezwa katika ukumbi wa Kasarani. Licha ya Senegal kuanza mechi hiyo kwa kasi, Kenya ilijikakamua na kushinda seti ya kwanza kwa alama 25-17. Katika seti ya pili Kenya haikua na kibarua na mashambulizi ya chipukizi hao yakaipa Kenya ushindi wa seti hiyo kwa alama 25-7. Kwenye seti ya tatu kenya ilizoa alama 25-8 na kuibuka ma iushindi wa mechi hiyo. kwenye mechi ya awali timu ya Misri ilipata ushindi wa seti 3-0 dhidi ya Rwanda.