.
11th September, 2016
Vyama vya wafanyikazi nchini vimeilaumu serikali ya Jubilee kwa kuanza kampeni za mapema na kusisitiza kuwa hatua hiyo itavuruga uchumi wa Kenya. Wakizungumza katika mazishi ya aliyekuwa kiongozi wa wafanyikazi halikadhalika waziri msaidizi Dennis Okumu, katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli na mwenzake wa KNUT Wilson Sossion walisema kwamba CORD na Jubilee wanastahili kujiepusha na kampeni za mapema na badala yake washughulikia majukumu yao ya kimsingi.