6th December, 2019
Zaidi ya mawakala elfu moja mia mbili walikongamana jijini Nairobi hapo jana kuadhimisha miaka miwili ya utendakazi wa muungano wa mawakala nchini. Kwenye kongamano hilo ajenda kuu ilifungamana na mazingira mazuri ya utendakazi na changamoto wanazokumbana nazo. Muungano huo unapania kuboresha utendakazi kwa wafanyakazi na mawakala wa kampuni za bima nchini.