×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Rais Uhuru Kenyatta apendekeza bunge kupunguza ushuru kwa bidhaa za mafuta

14th September, 2018

Rais Uhuru Kenyatta amehutubia taifa alasiri hii na kusema kwamba amependekezea bunge kupunguza ushuru wa thamani ya ziada kwa bidhaa za mafuta kutoka asilimia kumi na sita hadi asilimia nane. 

Rais amesema kwamba anaelewa mzigo wa gharama ya maisha ambayo Wakenya wanapambana nayo lakini akasisitiza kwamba ushuru huo unatokana na mswada uliopitishwa na bunge mwaka wa 2013. 

Aidha rais amesema kwamba kutokana na katiba mpya, nyadhifa kadhaa za uwakilishi zilibuniwa, na ndiposa gharama ya matumizi ya fedha imeongezeka.

.
RELATED VIDEOS