13th March, 2018
Polisi katika eneo bunge la Kiambaa eneo la Ndenderu wanachunguza mauaji ya watu wawili wa familia moja mbali na visa vingine vinavyoonekana kukithiri eneo hilo. Muuguzi katika hospitali ya St. Teresa Kikuyu alipatikana ameuwawa mita chache kutoka nyumbani kwake huku mwili wa mjombake Kenneth Warunge ukipatikana hatua chache kutoka kituo cha Ndenderu. Wawili hao wanadaiwa kuuwawa kwa kifaa butu kilichotumiwa kuwagonga kichwani.