.
26th January, 2022
Upasuaji wa miili ishirini na nne iliyopatikana katika mto Yala kuanzia mwezi oktoba mwaka jana ulianza leo katika hospitali ya Yala, huku familia zilizotambua miili ya jamaa zao zikihitajika kusubiri hadi wiki mbili zijazo kwa matokeo ya chembechembe za DNA.
Na sasa viongozi na mashirika ya kutetea haki za binadamu wanaitaka serikali kuweka mpango wa kukusanya chembechembe za DNA wakati wa kuzuiliwa ili kusaidia katika kumtambua yule aliyeaga ama kupotea.