.
3rd December, 2021
Mkurugenzi wa mashtaka ya umma Noordin Naji anasema kwamba kusafirishwa kwa aliyekuwa waziri wa fedha Chris Okemo na pamoja na mkurugenzi wa zamani wa kampuni ya kusambaza umeme nchini Samuel Gichuru hadi kisiwa cha Jersey ambako wana kesi ya kujibu, huenda itachukua muda zaidi. Haji amedokeza kwamba kisiwa hicho pamoja na tume ya kupambana na ufisadi nchini EACC, wataendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na kesi hiyo na huenda mengi zaidi yatajitokeza.