.
3rd December, 2021
Shughuli za uokoaji zinaendelea ili kuwanusuru wachimbaji wanane wa madini waliokwama katika mgodi mmoja wa kuchimba dhahabu baada ya kuta zake kuporomoka jana katika eneo la abimbo eneo la bondo kaunti ya siaya. Maafisa kutoka shirika la msalaba mwekundu wakishirikiana na maafisa wa kaunti ya siaya wameongoza jitihada za uokozi. Wachimbaji wawili walinusurika baada ya kupata majeraha madogo.