12th June, 2021
Ulimwengu ulipokuwa unaadhimisha siku ya kimataifa ya utoshelevu wa vyakula mapema wiki hii, utoshelezaji wa chakula umepewa kipaumbele haswa ikizingatiwa kuwa baadhi ya sehemu nchini zingali zinahangaishwa na baa la njaa. Ni kwa msingi hiyo ambapo sasa baadhi ya viongozi na mashirika yanajitokeza kuhakikisha kuwa wananchi wana chakula cha kutosha na maji kwa matumizi kama vile upanzi cha chakula.