.
12th June, 2021
Kwingineko, serikali ya kaunti ya Siaya imetoa wito kwa viongozi wa siasa na vilevile viongozi kwa jumla kutoka kaunti hiyo kusaidia katika vita dhidi ya maambukizi ya virusi vya korona kwa kutohudhuria hafla ambazo zina uwezo wa kuvutia umati mkubwa wa watu kama vile mazishi. Serikali hiyo inasema kwamba hafla hizi zimechangia pakubwa katika viwango vya juu vya maambukizi katika eneo la ziwa victoria haswa kaunti hiyo. Yanajiri hayo huku kaunti kutoka eneo hilo la ziwa zikiendelea kuongoza katika idadi ya maambukizi mapya ya virusi vya korona nchini.