.
9th June, 2021
Katibu mkuu wa chama cha Jubilee Raphael Tuju sasa anadai kuwa migogoro ambayo imekuwa ikishuhudiwa katika chama cha Jubilee imechochewa na ukabila. Tuju amekanusha shutuma kwamba yeye ni mmoja wa viongozi ambao wamefanya chama hicho kikose mwelekeo akisema kuwa chamgamoto kuu imekuwa ni ukabila akidai kuwa kumekuwa na jaribio la kumg’oa mamlakani kwa misingi ya kabila lake. Chama hicho sasa kinajiandaaa kufanya uchaguzi wa mashinani hadi afisi za kitaifa hivi karibuni.