.
9th June, 2021
Aliyekuwa Jaji Mkuu David Maraga amejitokeza hadharani na kuonya kuwa huenda taifa la Kenya likatumbukia katika machafuko na utawala usiozingatia utawala wa sheria, iwapo Rais Uhuru Kenyatta na utawala wake utaendelea kupuuza maagizo ya mahakama. Kwenye mahojiano ya kipekee na Ktn News, Maraga anasema hatua ya Rais kuacha kuwateuwa majaji sita kwenye orodha ya majaji arobaini iliyowasilishwa kwake na tume ya kuwaajiri wafanyikazi wa mahakama JSC, ni sawa na kuwahukumu machoni pa umma bila kuwasikiza. Maraga amesema atamkumbuka Rais Uhuru Kenyatta kama kiongozi aliyedharau na kudhihaki sheria.