.
3rd May, 2021
Wao huondoka nchini ili kutafuta riziki himaya za milki ya Uarabu wakiwa na matumaini kwamba siku moja watarejea tena nyumbani salama salmin. Hata hivyo, kwa baadhi yao azma hii ya kuisaka siku njema maishani inaendelea kugeuka tanzia kila uchao. Kumekuwa na ongezeko la visa vya ukiukaji wa haki za binadamu, dhulma za kimapenzi, mateso na hata sasa mauaji. Slaida Vugutsa Talian ndo mkenya wa hivi kupatikana akiwa ameuwa nchini Saudi Arabia, ambaye yamkini amekuwa akiandamwa na bahati mbaya hata baada ya kufariki. Hii leo tumekuandalia makala maalum, riziki ya mauti naye Duncan Khaemba.