.
7th April, 2021
Seneta wa Garissa Abdul Haji amesema kwamba anawezana na changamoto zinawazowakabili wakazi wa kaunti ya Garissa, baada ya kutawazwa seneta na tume ya Iebc hapo jana. Akizungumza kwenye mahojiano ya kipekee na Ktn News, Abdul Haji aliyerithishwa nafasi hio kufuatia kifo cha babake marehemu Yusuf Hajj alisema uteuzi wake ulitokana na maelewano ya wagombea na wazee wa jamii yake. Ameahidi kuutekeleza wajibu wake bila kumbagua yeyote kaunti ya Garissa.