.
7th April, 2021
Familia moja kutoka eneo la Likuyani kaunti ya Kakamega inaomboleza kifo cha mtoto wao aliyepigwa risasi na waasi ambao wanapinga serikali ya Sudan Kusini. Elijah Thiru ni miongoni mwa dereva 20 waliouliwa kwenye misururu ya mauaji katika barabara ya Juba?Nimule na Juba?Yei Sudan Kusini. Haya yamejiri huku muungano wa madereva wa masafa marefu nchini kenya ukiulaumu serikali kwa madai ya kushindwa kuwalinda madereva wakenya ambao maisha yao yamo hatarani nchini Sudan Kusini.