18th February, 2021
Familia moja katika eneo la mbale kaunti ya vihiga imesalia katika njia panda baada ya serikali ya kaunti hiyo kuwazuia kumzika mpendwa wao kwa zaidi ya miezi mitatu sasa kutokana na mzozo wa ardhi. familia hiyo imeshindwa kulipia ada ya chumba cha kuhifadhi maiti wakihofia huenda mzozo huo ukaendelea kwa muda mrefu. polisi walifika nyumbani siku ya maziko na kusisitiza mwendazake hafai kuzikwa katika boma hilo.