.
23rd January, 2021
Waziri wa usalama wa kitaifa Dkt Fred Matiang'i amesema kuwa viongozi ambao wamehusika katika mzozo ulioko Kapedo ambao ulichangia mauaji ya maafisa wa polisi watakamatwa. Matiangi alisema hayo katika sherehe ya shukrani ya naibu kamishna wa magereza Florence Omundi katika kijiji cha nyamache kaunti ya kisii na kuongeza kuwa ni aibu kwa viongozi kuwachochea wakazi.