.
4th December, 2020
Azma ya seneta wa Baringo Gideon Moi kuwania kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2022 hii leo imepigwa jeki, baada ya kiongozi wa chama cha mashinani Isaac Rutto, kutangaza kuwa chama chake hakitakuwa na mgombea wa urais na badala yake kumuunga mkono Gideon. Haya yamejiri huku baadhi ya viongozi wa bonde la ufa wakimtaka naibu wa rais William Ruto kutangaza wazi kuwa atapinga mchakato wa marekebisho ya katiba chini ya BBI.