.
31st October, 2020
Balozi mteule wa Kenya nchini Burundi Daniel Wambura hapo jana alikuwa na wakati mgumu mbele ya kamati ya bunge inayopiga msasa mabalozi wateule kuhusu utendakazi wake kama kamishna kwenye tume ya uchaguzi iliyotumbukiza nchi kwenye machafuko mwaka wa 2008 baada ya kutangaza matokeo ya kura ya urais. wambura alijitetea kwa kusema kwamba tume ya kriegler ilisema utepetevu kwenye asasi kadhaa za serikali ndio ulisababisha machafuko. wabunge pia walilumbana vikali kuhusu busara ya rais uhuru kenyatta kuteua baadhi ya watumishi wa umma ambao wamefikisha umri wa kustaafu kwa ubalozi.