.
30th September, 2020
Inaonekana ushindani wa utendakazi baina ya gavana wa kaunti ya Nairobi Mike Sonko na mkurugenzi wa NMS Mohammed Badi utaendelea wakati gavana Sonko akidai kuwa Badi anajaribu kuyafufua makundi ya watu wenye ushawishi katika City Hall. Kupitia msemaji wake Ben Mulwa, Sonko anadai NMS limeshindwa kutoa huduma na inakuja na mbinu za hujuma na hata hawafuati sheria.