.
9th December, 2019
Baada ya siku nne ya shughuli ya kuchimbua vifusi ili kuokoa waliokwama ndani katika eneo la mkasa wa kupromoka kwa jumba Tasia, kikosi cha pamoja kinachoendeleza shughuli hiyo kinasema shughuli hiyo sasa imekamilika. Kulingana na ripoti ya shirika la msalaba mwekundu, takriban watu 10 wamethibitishwa kufariki kutokana na mkasa huo na wengine 36 kuokolewa kutoka kwa vifusi vya jengo hilo. Waathiriwa wa mkasa huo sasa wamepewa hifadhi ya muda katika kanisa la kikatoliki la Taasia.