.
16th April, 2019
Hospitali katika baadhi ya kaunti zinakabiliwa na tishio la uhaba wa dawa, iwapo shirika la serikali la kuuza na kusambaza dawa kemsa, litasitisha huduma zake kwa kaunti kutokana na deni la shilingi bilioni mbili nukta tatu. Kaunti ya nairobi ndiyo imeorodhesha ya kwanza ikiwa na deni la shilingi milioni mia mbili na themanini na nne.